Uchanganuzi wa Makosa ya Kimofofonolojia Miongoni mwa Wanafunzi wa Kitachoni Wanapojifunza Kiswahili kama Lugha ya Pili
DOI:
https://doi.org/10.2026/jss.v3i1.12Keywords:
IstilahiMaalum: Lugha ya kwanza, Lugha ya pili, UchanganuziMakosa,Mofofonolojia,Mtalaa wa Umilisi na Utendaji.Abstract
IKISIRI
Wazungumzi wa lugha ya Kiswahili ambao lugha yao ya kwanza ni Kitachoni hufanya makosa katika
maandishi na matamshi yao kwa lugha ya Kiswahili.Makala haya yamefafanua makosa ya kimofofonolojia
miongoni mwa wanafunzi wanaozungumza Kitachoni wanapojifunza Kiswahili kama lugha yao ya
pili.Wanafunzi lengwa walikuwa wa kiwango cha gredi ya 7 na 8 walio ndani ya mtaala unaojikita katika
misingi ya Umilisi na Utendaji (Competency Based Education (CBE). Lengo mahsusi la kuyafafanua
makosa yaliyofanywa na wanafunzi hawa ni kuweka wazi michakato mahsusi ya kimofofonolojia inayo -
dhihirika na kupendekeza njia za kutatua kitaaluma. Uchunguzi huu uliongozwa na nadharia ya Uchanganuzi
makosa iliyoasisiwa na Corder (1967) kama mwongozo wa kuchambua makosa yaliyofanywa na
wanafunzi wateule katika gredi ya 7 na 8 na kisha kupendekeza njia mwafaka za kuwaepusha wasomaji
hawa kuyafanya makosa ya kimofofonolojia katika kazi zao za kimaandishi na pia za kimazungumzo.
Kutokana na udurusu wetu maktabani tulibaini kuwa kuna pengo la kiisimu katika ulinganishi wa lugha
ya Kitachoni ambayo ni lugha ya kwanza kwa lugha ya Kiswahili kama lugha ya pili na jambo hili ndilo
References
MAREJELEO
Corder, S. (1967) Error Analysis: Perspective
on the second language acquisition. London:
Longman.
Interlanguage: Oxford University Press.
Habwe, J., and P. Karanja. (2004) Misingi ya
Saru ya Kiswahili. Phoenix Publishers Ltd.,
Nairobi.
Hooper, J. B. (1976). An introduction to natural
g e n e r a t i v e p h o n o logy. Academic Press
Sounds, Sound Changes, and Words. Nairobi:
Focus publishers
Mgullu, R.S. (1999). Mtalaa wa Isimu: Fonetiki,
Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili. Nairobi:
Longhorn Publishers (K) Ltd.
Downloads
Published
How to Cite
Issue
Section
License
Copyright (c) 2026 Journal of Swahili Studies

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial 4.0 International License.